30/07/2022
DIMANCHE, TAREHE 31/07/2022
UKARIMU KATIKA NYAKATI ZA HATARI KUBWA
(1Wafalme 18: 3, 4)
“Ahaba akamuita Obadia aliekuwa juu ya nyumba yake. Naye Obadia alikuwa mtu mwenye kuogopa Bwana kabisa. Wakati Yezebeli alipoua manabii ya Bwana, Obadia alitwaa manabii mia moja, akawaficha makumi tano makumi tano katika pango, akawakulisha chakula na kuwapa maji.”
Ukichunguza mafungu haya mawili kwa njia ya kiroho, utatambua haraka ya kwamba Obadia ni mtu ambae alimtumainia Bwana. Alimuabudu Mungu na Mungu alibaki msingi wa matendo yake mema kwa jinsi alivyowaficha manabii mia moja katika pango ambapo alikuwa akiwahudumia.
Uaminifu na kazi yake vina chanzo katika kumutumainia Bwana tangu utoto wake (1Wafalme 18: 12). Wale ambao wanamwabudu Mungu kwa kweli, ndio pekee yao wanaoweza kutenda haki. Mawakili wa Bwana wanapashwa kuabudu kwa kweli na kuwa watumishi wa Bwana. Hili linawezekana wakati tunakubali faida zetu zibariki wengine. Mwezi huu wa zaka za chunguchungu, Mungu anakuomba ili uaminifu wako uweze kuchangia katika wokovu wa roho nyingi. Uaminifu wa Obadia ulionekana wakati wa kutisha kwa manabii wa Mungu.
Wakati Yezebeli aliwaua manabii wa Bwana, Obadia aliokoa na kuwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili (makumi tano fasi moja na makumi tano wengine fasi nyingine) tena alikuwa akiwatolea mkate na maji. Unawaza ya kwamba Obadia alitoa zaka za chunguchungu zapata je, alipolisha watu mia moja kila siku?
Kuficha watu mia moja katika pango na kuwapa chakula na maji siyo kazi rahisi. Hii inafaa tu kwa mtu aliyejitolea tena mwaminifu ili atimize tendo k**a hili. Hili haliwezi tendeka kwa njia ya mwili na damu, ila ni kwa njia ya Roho wa Bwana maishani mwetu. Hii inamaanisha ya kwamba Obadia alitumia pato lake, yaani alielewa ya kwamba vyote alivyo navyo ni vya Mungu ndipo akaamua kuvitoa kwa ajili ya kuokoa manabii wa Bwana. Hakika, huwezi kutimiza tendo hili ikiwa ungali unagangania mali ya Bwana na kuiita mali yako.
Obadia alitumia mali yake na kupangil