31/03/2022
∆YEREMIA 9:23
BWANA ASEMA HIVI,MWENYE HEKIMA ASIJISIFU KWA SABABU YA HEKIMA YAKE,WALA MWENYE NGUVU ASIJISIFU KWA SABABU YA NGUVU ZAKE,WALA TAJIRI ASIJISIFU KWA SABABU YA UTAJIRI WAKE,BALI AJISIFUYE NA AJISIFU KWA SABABU HII:YA KWAMBA ANANIFAHAMU MIMI,NA KUNIJUWA ,YA KUWA MIMI NI BWANA NITENDAYE WEMA,NA HUKUMU NA HAKI KATIKA INCHI MAANA MIMI NAPENDEZWA NA MAMBO HAYO,ASEMA BWANA.
Katika maisha ya watu wengi kuna vitu ambavyo wamevipa kipaumbele na kujisifu kwa sababu y'a vitu hivyo wakati vitu hivyo havita wafikisha popote,na vimefanya wawe na kiburi na kuwaona wengine k**a hawafai wakati wameacha kitu cha msingi na cha maana katika maisha yao.
Mtu ambaye ana hekima kwa jambo fulani ametaka awe mkuu juu y'a wengine na kujisifu kwa sababu ya hekima yake, wakati hekima maandiko inasema hekima ya dunia hii ni upumbavu mbele za Mungu,na inaendeleya kusema k**a usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.Kumbe ili tuitwe wenye hekima lazima tuwe wapumbavu kwa dunia ili Mungu atuelimishe,kumbe hekima si kitu bila kumjuwa Mungu.
Mwenye nguvu ni nani k**a haiko yule ambaye amemjuwa Mungu kweli kweli? K**a haumjuwe Mungu wewe ni dhaifu hâta k**a ungekuwa mrefu kiasi gani,mnene kiasi gani mwenye misuri kiasi gani wewe ni mnyonge kabisa,waza DAUDI ALIMUUAJE GOLIATH ?
Utaji bila Mungu ni umaskini kweli kweli kwa maana hauta fikisha roho yako popote,hauwezi kukupa uzima,amani na furaha ya kweli alité tajiri ni yule ambaye amemjuwa Mungu katika WEMA HAKI NA HUKUMU YA KWELI,kwa maana imeandikwa UFALME WA MUNGU SI KULA NA KUNYWA BALI HAKI FURAHA NA AMANI
MUNGU AKUBARIKI NA AKUPE NEEMA YA KUMJUWA YEYE
Giscard mose