29/09/2025
*MAANA YA DUA*
Dua au maombi maana yake, ni mja kudhihirisha na kuyaweka wazi
mahitaji yake mbele ya hadhara tukufu ya Mwenyezi Mungu ambaye
si muhitaji kwa yeyote.
Dua ni pale mja anapojieleza kuwa yeye ni muhitaji, dhaifu tena
mnyonge. Yote haya akayaaridhi mbele ya hadhara ya Mwenyezi
Mungu ambaye ndiye mwenye mamlaka katika ulimwengu wote na
ndiye mkwasi asiyefilisika.
Dua ni kitendo cha mja kunyanyua mikono yake na kukunjua viganja
vyake vitupu visivyokuwa na kitu, kisha akavielekeza kwa Mwenyezi
Mungu ambaye ni Mkarimu.
Si hivyo tu, bali kwa kufanya hivyo akaonesha wazi namna
asivyokuwa na uwezo mbele ya Mwenyezi Mungu Muweza
Aliyetukuka.
Dua ni maombi ya mja masikini, dhalili na fukara anayetaka msaada
kwa Mwenyezi Mungu Muumba Mwenye huruma, Mpole Mwenye
kusikia na Mwenye kuona.
Dua ni kudhihirisha unyenyekevu na udhalili wa mja mbele ya
hadhara tukufu ya Mwenyezi Mungu ambaye ni Mfalme Mwenye
Utukufu, Mwenye nguvu na Mjuzi mno.
Dua ni lugha ya upendo inayotumika baina ya mja na Mola wake
Mwenye mapenzi kwa waja wake. Dua ni chemchem inayotiririka
kutoka kwa waja wa Mwenyezi Mungu wanaompenda. Dua
ni kiliwazo cha wachamungu, ni taa inayowaka kuwamulikia
wanaosafiri safari ya kiroho kumwendea Mola wao, na ni nguzo ya
masikini na wenye shida.Bali dua ni nuru inayo ng’ara ndani ya nyoyo za watu wanao tanga
tanga wakitafuta kuokolewa!
By _mustafa lokol_ *0785774494*